MAISHA HALISI YA MTOTO NA KIJANA WA MTAANI.

 


Kitabu hiki cha maisha halisi ya mtoto wa mtaani ni ushuhuda wa kweli wa JAMES YUSTAR JUSTINE EBRANIA, aliyeokotwa jalalani na baada ya safari ndefu ya maisha yake toka kuokotwa kwake, kupitia mazingira magumu hatari na yenye misukosuko mingi. James aanza maisha mapya na kuweka historia kati ya walioshinda maisha ya kuitwa watoto wa mitaani.
 
Kitabu hiki kinatoa Taswira ya mabadiliko kwa jamii iliyokata tamaa pia kinaelezea mazingira halisi ya watoto wa mtaani, matatizo na maisha magumu wanayoyapitia kama unyanywasaji, njaa, vifo, majeraha, hata ulemavu wa kudumu, ukosefu wa elimu, huduma muhimu, ukosefu wa elimu, hudumu muhimu za kijamii kama matibabu na malazi bora.
 
Kwa kupitia kitabu hiki kinachoelezea maisha halisi ya James Yuster kinaonyesha kwa hisia jinsi watoto wa mtaani wanavyojihisi / kujiona kuwa jamii imewatenga wananyanyapaliwa na kujihisi upweke, kana kwamba hawana haki ya kuhishi pamoja na jamii hapa Duniani.
 
Pia utapata kuona jinsi hawa watoto walivyosahaulika katika jamii na kupoteza thamani ya utu wao, jamii inawachukulia kama wezi, wahuni, watumiaji wa dawa za kulevya, ulawiti na kuonekana kama viumbe wa ajabu machoni mwao.
 
Kupitia kitabu hiki jamaii itajifunza madhara ya utoaji mimba na utupaji wa watoto ambao hupelekea ongezeko la watoto wa mtaani, hivyo nivyema jamii ikaelimika na kushiriki katika kupunguza kundi kubwa la watoto wanaoishi katika mazingira magumu. 
 
-------------------------------------------------------------

This book on the real-life story of a street child is a true testimony of JAMES YUSTAR JUSTINE EBRANIA, who was found abandoned at a dumpsite. After a long and difficult life journey—facing dangerous and challenging circumstances—James eventually began a new life and made history as one of the few who overcame the label of a street child.

This book offers a vivid portrayal of transformation for a society that has lost hope. It also describes the harsh reality faced by street children, including abuse, hunger, death, injuries, even permanent disabilities, lack of education, and the absence of essential social services such as healthcare and proper shelter.

Through this book, which narrates the true experiences of James Yustar, readers will emotionally connect with how street children feel neglected, stigmatized, and isolated—as though they have no right to exist within society.

You will also see how these children are forgotten by society and stripped of their dignity. They are often perceived as thieves, troublemakers, drug addicts, or victims of sexual abuse, and viewed as strange beings in the eyes of many.

This book also aims to educate society on the consequences of abortion and child abandonment—factors that contribute to the increasing number of street children. Therefore, it is vital for communities to be educated and actively involved in reducing the population of children living in vulnerable conditions.


Post a Comment

0 Comments